student expert

Kuwa mwanafunzi mtaalam wa COVID-19

Ni nini tofauti kati ya virusi vya Corona na COVID-19?

Virusi vya Corona ni familia ya virusi ambavyo vinaweza kusababisha magonjwa kwa wanadamu. COVID-19, pamoja na SARS na MERS, ni moja ya virusi vingi katika familia hii ambavyo vinaweza kusababisha shida ya kupumua.

Ni zipi dalili za COVID-19?

  • Homa
  • Kuvuta kamasi
  • Kikohozi
  • Uchovu
  • Upungufu wa pumzi

COVID-19 inaenea vipi?

COVID-19 inaenea kupitia pumzi yako katika matone madogo ambayo huwezi kuona. Wakati mtu anapopumua, kukohoa, au kupiga chafya matone haya yanawekwa kwenye hewa na mtu mwingine anaweza kuyapumua. Wakati matone yanaanguka kutoka hewani yanaweza ishi pia kwenye sehemu,mahali mtu anaweza kuyaguza na kisha kugusa uso, mdomo, macho au pua. Hii ndio sababu kujitenga kijamii na kuosha mikono yako mara kwa mara kwa sabuni na maji ni muhimu.

Janga ni nini?

Shirika la Afya Ulimwenguni, au WHO, lilitangaza COVID-19 kuwa janga la ulimwengu mnamo Machi 12, 2020. Hii inamaanisha ugonjwa umeenea kote ulimwenguni kwa nchi tofauti kwenye mabara mengi.

Umbali wa kijamii ni nini?

Kudumisha umbali wa kijamii kunamaanisha kuepuka mikusanyiko mikubwa na kudumisha angalau umbali wa fiti 3, au mita 1, kutoka kwa wengine ili kuzuia kuenea kwa COVID-19. Kwa kuongeza, unapomsalimia mtu dumisha umbali huo na epuka kutikisa mikono, kubusu na kukumbatiana. Epuka kutumia matumizi ya usafiri wa umma na kama unahisi vibaya kaa nyumbani. Kwa bahati mbaya, hii pia ni pamoja na mtu wa familia na marafiki ambao unaishi nao. Wasiliana na kila mmoja kwa kutumia teknolojia kama vile simu na mtandao wa kijamii

Kutoonyesha dalili inamaanisha nini?

Kutoonyesha dalili inamaanisha mtu anahisi na anaonekana mwenye afya lakini ana virusi na bado anaweza kuambukiza. Hata watu wenye dalili wanaweza kueneza COVID-19, ambayo ni sababu nyingine kufanya mazoezi ya kujitenga kijamii.

COVID-19 inachukua muda gani na ni lini naweza kuambukizwa?

Dalili kawaida hudumu kwa siku 5-7 lakini unaweza eneza ugonjwa siku 2 - 14 kabla ujihisi mgonjwa. Walakini,watu wanawezakuwa wagonjwa kwa wiki mbili au zaidi, kulingana na umri wa mtu na hali yake ya matibabu. Watu wanaohisi wagonjwa wanapaswa kwenda kujipeleka karantini.

Nifanye nini na habari hii?

Sasa kwa kuwa wewe ni mtaalam, shiriki maarifa yako mapya na marafiki na familia!

Ifuatayo